Isaya 42

Mtumishi Wa Bwana

1 “Huyu hapa mtumishi wangu, ninayemtegemeza,

mteule wangu, ambaye ninapendezwa naye;

nitaweka Roho yangu juu yake,

naye ataleta haki kwa mataifa.

2 Hatapaza sauti wala kupiga kelele,

wala hataiinua sauti yake barabarani.

3 Mwanzi uliopondeka hatauvunja

na utambi ufukao moshi hatauzima.

Kwa uaminifu ataleta haki,

4 hatazimia roho wala kukata tamaa

mpaka atakaposimamisha haki juu ya dunia.

Visiwa vitaweka tumaini lake katika sheria yake.”

5 Hili ndilo asemalo Mungu,Bwana,

yeye aliyeziumba mbingu na kuzitanda,

aliyeitandaza dunia na vyote vitokavyo humo,

awapaye watu wake pumzi

na uzima kwa wale waendao humo:

6 “Mimi,Bwana, nimekuita katika haki;

nitakushika mkono wako.

Nitakulinda na kukufanya

kuwa Agano kwa ajili ya watu

na nuru kwa Mataifa,

7 kuwafungua macho wale wasioona,

kuwaacha huru kutoka kifungoni waliofungwa jela,

na kuwafungua kutoka gerezani

wale wanaokaa gizani.

8 “Mimi ndimiBwana; hilo ndilo Jina langu!

Sitampa mwingine utukufu wangu

wala sanamu sifa zangu.

9 Tazama, mambo ya kwanza yametokea,

nami natangaza mambo mapya;

kabla hayajatokea

nawatangazia habari zake.”

Wimbo Wa Kumsifu Bwana

10 MwimbieniBwanawimbo mpya,

sifa zake toka miisho ya dunia,

ninyi mshukao chini baharini,

na vyote vilivyomo ndani yake,

enyi visiwa na wote wakaao ndani yake.

11 Jangwa na miji yake na vipaze sauti zao;

makao anamoishi Kedari na yashangilie.

Watu wa Sela waimbe kwa furaha

na wapige kelele kutoka vilele vya milima.

12 WampeBwanautukufu

na kutangaza sifa zake katika visiwa.

13 Bwanaataenda kama mtu mwenye nguvu,

kama shujaa atachochea shauku yake,

kwa kelele ataamsha kilio cha vita

naye atashinda adui zake.

14 “Kwa muda mrefu nimenyamaza kimya,

nimekaa kimya na kujizuia.

Lakini sasa, kama mwanamke wakati wa kujifungua,

ninapiga kelele, ninatweta

na kushusha pumzi.

15 Nitaharibu milima na vilima

na kukausha uoto wake wote;

nitafanya mito kuwa visiwa

na kukausha mabwawa.

16 Nitawaongoza vipofu kwenye njia ambayo hawajaijua,

kwenye mapito wasiyoyazoea nitawaongoza;

nitafanya giza kuwa nuru mbele yao

na kufanya mahali palipoparuza kuwa laini.

Haya ndiyo mambo nitakayofanya;

mimi sitawaacha.

17 Lakini wale wanaotumaini sanamu,

wanaoviambia vinyago, ‘Ninyi ndio miungu yetu,’

watarudishwa nyuma kwa aibu kubwa.

Israeli Kipofu Na Kiziwi

18 “Sikieni, enyi viziwi;

tazameni, enyi vipofu, mpate kuona!

19 Ni nani aliye kipofu isipokuwa mtumishi wangu,

na kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?

Ni nani aliye kipofu kama yeye aliyejitoa kwangu,

aliye kipofu kama mtumishi waBwana?

20 Mmeona vitu vingi, lakini hamkuzingatia;

masikio yenu yako wazi lakini hamsikii cho chote.”

21 IlimpendezaBwana

kwa ajili ya haki yake

kufanya sheria yake kuwa kuu na tukufu.

22 Lakini hili ni taifa lililoibwa na kutekwa nyara,

wote wamenaswa katika mashimo,

au wamefichwa katika magereza.

Wamekuwa nyara,

wala hapana ye yote awaokoaye.

Wamefanywa mateka,

wala hapana ye yote asemaye, “Warudishe.”

23 Ni nani miongoni mwenu atakayesikiliza hili

au atakayezingatia kwa makini katika wakati ujao?

24 Ni nani aliyemtoa Yakobo kuwa mateka,

na Israeli kwa wateka nyara?

Je, hakuwaBwana,

ambaye tumetenda dhambi dhidi yake?

Kwa kuwa hawakufuata njia zake,

hawakutii sheria zake.

25 Hivyo akawamwagia hasira yake inayowaka,

ukali wa vita.

Ikawazunguka kwa miali ya moto,

hata hivyo hawakuelewa;

ikawateketeza,

lakini hawakuyatia moyoni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/42-788fb4b293f8b7e54626fd900a3a74bd.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

thirteen − 6 =