Yeremia 36

Yehoyakimu Achoma Kitabu Cha Yeremia

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwaBwanakusema:

2 “Chukua kitabu na uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.

3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo kila mmoja wao atageuka kutoka katika njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”

4 Hivyo Yeremia akamwita Baruki mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasemaBwana, Baruki akayaandika katika kitabu.

5 Kisha Yeremia akamwambia Baruki, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu laBwana.

6 Basi wewe nenda katika nyumba yaBwanasiku ya kufunga na uwasomee watu maneno yaBwanakutoka katika kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka kwenye miji yao.

7 Labda wataomba na kusihi mbele zaBwanana kila mmoja atageuka kutoka katika njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa naBwanani kubwa.”

8 Baruki mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya, katika Hekalu laBwanaalisoma maneno yaBwanakutoka katika kile kitabu.

9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele zaBwanailitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.

10 Kutoka katika chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruki akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu laBwanamaneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.

11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote yaBwanakutoka kwenye kile kitabu,

12 alishuka kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote, yaani: Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania na maafisa wengine wote.

13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruki akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,

14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruki, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruki mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.

15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.”

Ndipo Baruki akawasomea kile kitabu.

16 Walipoyasikia maneno haya yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruki, “Ni lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”

17 Kisha wakamwuliza Baruki, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”

18 Baruki akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”

19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruki, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu ye yote asijue mahali mlipo.”

20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.

21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu na Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.

22 Ulikuwa mwezi wa tisa na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.

23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni hadi kitabu chote kikateketea.

24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yo yote wala hawakuyararua mavazi yao.

25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu lakini hakuwasikiliza.

26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruki na nabii Yeremia. LakiniBwanaalikuwa amewaficha.

27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruki aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno laBwanalilimjia Yeremia likisema:

28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.

29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemaloBwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”

30 Kwa hiyo, hili ndilo asemaloBwanakuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu ye yote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi, maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.

31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao, nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’ ”

32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruki mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruki akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto na maneno mengine mengi yanayofanana na hayo yaliyoongezewa humo.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/36-2fda8ecc95aeb8e760099e8bb2aca80c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fifteen − six =