Yeremia 50

Ujumbe Kuhusu Babeli

1 Hili ndilo neno alilosemaBwanakupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:

2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,

twekeni bendera na mkahubiri;

msiache kitu cho chote, bali semeni,

‘Babeli utatekwa;

Beli ataaibishwa,

Merodaki atajazwa na hofu kuu.

Sanamu zake zitaaibishwa

na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’

3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia

na kuifanya nchi yake ukiwa.

Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,

watu na wanyama wataikimbia.

4 “Katika siku hizo, wakati huo,”

asemaBwana,

“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda

wataenda wakilia

ili kumtafutaBwanaMungu wao.

5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni

na kuelekeza nyuso zao huko.

Watakuja na kuambatana naBwana

katika Agano la milele

ambalo halitasahaulika.

6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;

wachungaji wao wamewapotosha

na kuwasababisha kuzungukazunguka

juu ya milima.

Walitangatanga juu ya mlima na kilima

na kusahau mahali pao wenyewe

pa kupumzikia.

7 Ye yote aliyewakuta aliwala;

adui zao walisema,

‘Sisi hatuna hatia,

kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi yaBwana,

malisho yao halisi,

Bwana, aliye tumaini la baba zao.’

8 “Kimbieni kutoka Babeli;

ondokeni katika nchi ya Wakaldayo

tena iweni kama mbuzi wale waongozao kundi.

9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli

muungano wa mataifa makubwa

kutoka nchi ya kaskazini.

Watashika nafasi zao dhidi yake,

naye kwa kutokea kaskazini atatekwa.

Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari

ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.

10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;

wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”

asemaBwana.

11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi,

wewe utekaye urithi wangu,

kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka

na kulia kama farasi dume asiyehasiwa,

12 mama yako ataaibika mno,

yeye aliyekuzaa atatahayari.

Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,

atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.

13 Kwa sababu ya hasira yaBwanahatakaliwa na mtu,

lakini ataachwa ukiwa kabisa.

Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki

kwa sababu ya majeraha yake yote.

14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,

enyi nyote mvutao upinde.

Mpigeni! Msibakize mshale wo wote,

kwa kuwa ametenda dhambi dhidi yaBwana.

15 Piga kelele dhidi yake kila upande!

Anajisalimisha, minara yake inaanguka,

kuta zake zimebomoka.

Kwa kuwa hiki ni kisasi chaBwana,

mlipizeni kisasi;

mtendeeni kama alivyowatendea wengine.

16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,

naye mvunaji pamoja na mundu wake akivuna.

Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu

kila mmoja na arejee

kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja na akimbilie

kwenye nchi yake mwenyewe.

17 “Israeli ni kundi lililotawanyika

ambalo simba wamelifukuzia mbali.

Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,

wa mwisho kuponda mifupa yake

alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”

18 Kwa hiyo hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake

kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.

19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe

naye atalisha huko Karmeli na Bashani;

njaa yake itashibishwa

juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.

20 Katika siku hizo, wakati huo,”

asemaBwana,

“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,

lakini halitakuwepo,

kwa ajili ya dhambi za Yuda,

lakini haitapatikana hata moja,

kwa kuwa nitawasamehe

mabaki nitakaowaacha.

21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu

na wale waishio huko Pekodi.

Wafuatieni, waueni

na kuwaangamiza kabisa,”

asemaBwana.

“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.

22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi,

kelele ya maangamizi makuu!

23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote

ilivyovunjika na kuharibika!

Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa

miongoni mwa mataifa!

24 Nimetega mtego kwa ajili yako, Ee Babeli,

nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;

ulipatikana na ukakamatwa

kwa sababu ulimpingaBwana.

25 Bwanaamefungua ghala lake la silaha

na kuzitoa silaha za ghadhabu yake,

kwa kuwaBwanaMwenyezi Mwenye Nguvu Zote

anayo kazi ya kufanya

katika nchi ya Wakaldayo.

26 Njoni dhidi yake kutoka mbali.

Zifungueni ghala zake za nafaka;

mlundikeni kama lundo la nafaka.

Mwangamizeni kabisa

na msimwachie mabaki yo yote.

27 Waueni mafahali wake wachanga wote;

waacheni washuke machinjoni!

Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,

wakati wao wa kuadhibiwa.

28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli

wakitangaza katika Sayuni

jinsiBwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,

wote wale wavutao upinde.

Pigeni kambi kumzunguka kabisa,

asitoroke mtu ye yote.

Mlipizeni kwa matendo yake;

mtendeeni kama alivyotenda.

Kwa kuwa alimdharauBwana,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”

asemaBwana.

31 “Tazama, niko kinyume nawe, Ewe mwenye majivuno,”

asema Bwana,BwanaMwenye Nguvu Zote,

“kwa kuwa siku yako imewadia,

yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.

32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,

wala hakuna ye yote atakayemuinua;

nitawasha moto katika miji yake,

utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

33 Hili ndilo asemaloBwanaMwenye Nguvu Zote:

“Watu wa Israeli wameonewa,

nao watu wa Yuda pia.

Wote waliowateka wamewashikilia sana,

wanakataa kuwaachia waende.

34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu;

BwanaMwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

Atatetea kwa nguvu shauri lao

ili kwamba alete raha katika nchi yao,

lakini ataleta msukosuko

kwa wale waishio Babeli.

35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!”

asemaBwana,

“dhidi ya wale waishio Babeli

na dhidi ya maafisa wake

na watu wenye busara!

36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!

Watakuwa wapumbavu.

Upanga dhidi ya mashujaa wake!

Watajazwa na hofu kuu

37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita

pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!

Wao watakuwa kama wanawake.

Upanga dhidi ya hazina zake!

Hizo zitatekwa nyara.

38 Ukame juu ya maji yake!

Nayo yatakauka.

Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,

wao wanapenda sana sanamu.

39 “Hivyo viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,

nao bundi watakaa humo.

Kamwe haitakaliwa tena

wala watu hawataishi humo

kutoka kizazi hadi kizazi.

40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora

pamoja na miji iliyo jirani nayo,”

asemaBwana,

“vivyo hivyo hapatakuwa na mtu ye yote

atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu ye yote

atakayekaa humo.

41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;

taifa kubwa na wafalme wengi

wameamshwa kutoka miisho ya dunia.

42 Wamejifunga pinde na mikuki;

ni wakatili na wasio na huruma.

Wanasikika kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao;

wanakuja kama watu waliojipanga kwa vita

ili kukushambulia, Ee Binti Babeli.

43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu hao,

nayo mikono yake imelegea.

Uchungu umemshika,

maumivu kama yale ya mwanamke

aliye katika utungu wa kuzaa.

44 Kama simba anayepanda kutoka kwenye vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho manono,

nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule,

nimweke kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi

awezaye kusimama dhidi yangu?”

45 Kwa hiyo, sikia kileBwanaalichokipanga dhidi ya Babeli,

kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali,

ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

46 Kwa kusikika kutekwa kwa Babeli,

dunia itatetemeka;

kilio chake kitaenea pote

miongoni mwa mataifa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/50-5b601e05cff5714c3c5f4e4f3abb1384.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

20 − sixteen =