Yoshua Anawaaga Viongozi
1 Baada ya muda mrefu kupita, nayeBwanaalikuwa amewapa Israeli raha mbele ya adui zao wote waliowazunguka, Yoshua, wakati huo alikuwa mzee na umri ukiwa umeendelea sana,
2 akawaita Israeli wote, wazee wao, viongozi, waamuzi na maafisa wao, na kuwaambia: “Mimi ni mzee na umri umeendelea sana.
3 Ninyi wenyewe mmeona kila kituBwanaMungu wenu, alichowatendea makabila haya yote kwa ajili yenu, ilikuwa niBwanaMungu wenu aliyewapigania.
4 Kumbukeni jinsi nilivyowagawia kama urithi kwa ajili ya makabila yenu yote nchi ya mataifa yaliyobaki, yaani mataifa niliyowashinda, kati ya Mto Yordani na Bahari ile kuu upande wa magharibi.
5 BwanaMungu wenu mwenyewe, atawaondoa watoke mbele yenu. Atawafukuza mbele yenu, nanyi mtamiliki nchi yao, kama vileBwanaMungu wenu alivyowaahidi.
6 “Iweni hodari sana, iweni waangalifu kutii yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Torati ya Mose, pasipo kugeuka upande wa kuume au kushoto.
7 Msishirikiane na mataifa yaliyobakia katikati yenu, wala msiombe kwa majina ya miungu yao au kuapa kwayo. Msiitumikie wala kuisujudia.
8 Bali mtashikamana kwa uthabiti na Mungu wenu, kama vile ambavyo mmefanya mpaka sasa.
9 “Bwanaamewafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu, mpaka siku ya leo hakuna ye yote aliyeweza kusimama mbele yenu.
10 Mtu mmoja miongoni mwenu atafukuza watu elfu, kwa kuwaBwanaMungu wenu anawapigania, kama alivyoahidi.
11 Kwa hiyo iweni waangalifu sana kumpendaBwanaMungu wenu.
12 “Lakini ikiwa mtageuka na kushikamana na mabaki ya mataifa haya yaliyosalia katikati yenu na kama mtaoana na kushirikiana nao,
13 basi mwe na hakika kuwaBwanaMungu wenu hatawafukuza tena mataifa hayo mbele yenu. Badala yake, watakuwa tanzi na mitego kwenu, mijeledi migongoni mwenu na miiba machoni penu, mpaka mwangamie kutoka katika nchi hii nzuri, ambayoBwanaMungu wenu amewapa.
14 “Sasa mimi ninakaribia kwenda katika njia ya watu wote wa dunia. Mnajua kwa mioyo yenu na roho zenu kwamba hakuna ahadi zo zote njemaBwanaMungu wenu alizowaahidia, ambazo hazikutimia. Kila ahadi imetimizwa, hakuna hata moja ambayo haikutimia.
15 Bali kama vile ambavyo kila ahadi njema yaBwanaMungu wenu imekuwa kweli, vivyo hivyoBwanaataleta maovu yote aliyosema, mpaka awe amewaangamiza kutoka katika nchi hii nzuri aliyowapa.
16 Kama mkilivunja Agano laBwanaMungu wenu, ambalo aliwaamuru ninyi, mkaenda na kuitumikia miungu mingine na kuisujudia, hasira yaBwanaitawaka dhidi yenu, nanyi mtaangamia mara kutoka katika nchi nzuri aliyowapa ninyi.”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JOS/23-66bad3d200ae96492b40ac9253ae7665.mp3?version_id=1627—