Dunia Yote Yaitwa Kumsifu Mungu
(Zaburi Ya Shukrani)
1 MpigieniBwanakelele za shangwe,
dunia yote.
2 MwabuduniBwanakwa furaha;
njoni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
3 Jueni kwambaBwanandiye Mungu.
Yeye ndiye aliyetuumba,
sisi tu mali yake;
sisi tu watu wake,
kondoo wa malisho yake.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
5 Kwa maanaBwanani mwema
na upendo wake wadumu milele;
uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/100-eff14a40452cabadf74ec057d9d8d961.mp3?version_id=1627—