Zaburi 100

Dunia Yote Yaitwa Kumsifu Mungu

(Zaburi Ya Shukrani)

1 MpigieniBwanakelele za shangwe,

dunia yote.

2 MwabuduniBwanakwa furaha;

njoni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.

3 Jueni kwambaBwanandiye Mungu.

Yeye ndiye aliyetuumba,

sisi tu mali yake;

sisi tu watu wake,

kondoo wa malisho yake.

4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani

na katika nyua zake kwa kusifu,

mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.

5 Kwa maanaBwanani mwema

na upendo wake wadumu milele;

uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/100-eff14a40452cabadf74ec057d9d8d961.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

17 + 20 =