Zaburi 101

Ahadi Ya Kuishi Kwa Uadilifu Na Kwa Haki

(Zaburi Ya Daudi)

1 Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako;

kwako wewe, EeBwana,

nitaimba sifa.

2 Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama:

utakuja kwangu lini?

Nitatembea nyumbani mwangu

kwa moyo usio na lawama.

3 Sitaweka mbele ya macho yangu

kitu kiovu.

Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani;

hawatashikamana nami.

4 Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami;

nitajitenga na kila ubaya.

5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri,

huyo nitamnyamazisha;

mwenye macho ya dharau

na moyo wa kiburi sitamvumilia.

6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,

ili waweze kuishi pamoja nami;

yeye ambaye moyo wake

hauna lawama atanitumikia.

7 Mdanganyifu hatakaa

nyumbani mwangu,

yeye asemaye kwa uongo

hatasimama mbele yangu.

8 Kila asubuhi nitawanyamazisha

waovu wote katika nchi;

nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya

kutoka katika mji waBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/101-94c837dab923fee4400aad2840d4c3c4.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

10 − 9 =