Zaburi 110

Bwana Na Mfalme Wake Mteule

(Zaburi Ya Daudi)

1 Bwanaamwambia Bwana wangu:

“Keti mkono wangu wa kuume,

mpaka nitakapowafanya adui zako

kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”

2 Bwanaataeneza fimbo yako ya utawala

yenye nguvu kutoka Sayuni;

utatawala katikati ya adui zako.

3 Askari wako watajitolea kwa moyo

katika siku yako ya vita.

Ukiwa umevikwa fahari takatifu,

kutoka kwenye tumbo la mapambazuko

# utapokea umande wa ujana wako.

4 Bwanaameapa,

naye hatabadilisha mawazo yake:

“Wewe ni kuhani milele,

kwa mfano wa Melkizedeki.”

5 Bwana yuko mkono wako wa kuume,

atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.

6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga

na kuwaponda watawala wa dunia nzima.

7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia,

kwa hiyo atainua kichwa chake juu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/110-8f324b599490c012590b4eb9baf7390b.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eleven − 4 =