Zaburi 113

Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake

1 MsifuniBwana.

Enyi watumishi waBwanamsifuni,

lisifuni jina laBwana.

2 Jina laBwanana lisifiwe,

sasa na hata milele.

3 Kuanzia maawio ya jua hadi machweo yake,

jina laBwanalinapaswa kusifiwa.

4 Bwanaametukuka juu ya mataifa yote,

utukufu wake juu ya mbingu.

5 Ni nani aliye kamaBwanaMungu wetu,

Yeye ambaye ameketi juu

kwenye kiti cha enzi,

6 ambaye huinama atazame chini

aone mbingu na nchi?

7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,

na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,

8 huwaketisha pamoja na wakuu,

pamoja na wakuu wa watu wake.

9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,

akiwa mama wa watoto mwenye furaha.

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/113-53c3869e1e1a9355715e21b5247d5f73.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 × 4 =