Zaburi 116

Shukrani Kwa Kuokolewa Kutoka Mautini

Sifa Kwa Mungu

1 NinampendaBwanakwa maana amesikia sauti yangu;

amesikia kilio changu ili anihurumie.

2 Kwa sababu amenitegea sikio lake,

nitamwita siku zote za maisha yangu.

3 Kamba za mauti zilinizunguka,

maumivu makuu ya kuzimu yalinipata,

nikalemewa na taabu na huzuni.

4 Ndipo nikaliitia jina laBwana:

“EeBwana, niokoe!”

5 Bwanani mwenye neema na haki,

Mungu wetu ni mwingi wa huruma.

6 Bwanahuwalinda wanyenyekevu,

nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.

7 Ee nafsi yangu, tulia tena,

kwa kuwaBwanaamekuwa mwema kwako.

8 Kwa kuwa wewe, EeBwana,

umeniokoa nafsi yangu na mauti,

macho yangu kutokana na machozi,

miguu yangu kutokana na kujikwaa,

9 ili niweze kutembea mbele zaBwana,

katika nchi ya walio hai.

10 Niliamini, kwa hiyo nilisema,

“Mimi nimeteseka sana.”

11 Katika taabu yangu nilisema,

“Wanadamu wote ni waongo.”

12 NimrudishieBwananini

kwa wema wake wote alionitendea?

13 Nitakiinua kikombe cha wokovu

na kulitangaza jina laBwana.

14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwaBwana

mbele za watu wake wote.

15 Kifo cha watakatifu kina thamani

machoni paBwana.

16 EeBwana, hakika mimi ni mtumishi wako,

mimi ni mtumishi wako,

# mwana wa mjakazi wako;

umeniweka huru

toka katika minyororo yangu.

17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru

na kuliita jina laBwana.

18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwaBwana

mbele za watu wake wote,

19 katika nyua za nyumba yaBwana,

katikati yako, Ee Yerusalemu.

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/116-426552c15b8abe3ec7a3067ce28fab59.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

three × 4 =