Shukrani Kwa Ajili Ya Ushindi
1 MshukuruniBwana, kwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
2 Israeli na aseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
3 Nyumba ya Aroni na iseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
4 Wote wamchaoBwanana waseme sasa:
“Upendo wake wadumu milele.”
5 Wakati wa maumivu yangu makuu nilimliliaBwana,
naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 Bwanayuko pamoja nami, sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 Bwanayuko pamoja nami,
yeye ni msaidizi wangu.
Nitawatazama adui zangu kwa furaha
wakiwa wameshindwa.
8 Ni bora kumkimbiliaBwana
kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 Ni bora kumkimbiliaBwana
kuliko kuwatumainia wakuu.
10 Mataifa yote yalinizunguka,
lakini kwa jina laBwananaliwakatilia mbali.
11 Walinizunguka pande zote,
lakini kwa jina laBwananaliwakatilia mbali.
12 Walinizunguka kama kundi la nyuki,
lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo;
kwa jina laBwananaliwakatilia mbali.
13 Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka,
lakiniBwanaalinisaidia.
14 Bwanani nguvu yangu na wimbo wangu,
yeye amefanyika wokovu wangu.
15 Sauti za shangwe na ushindi
zinavuma hemani mwa wenye haki:
“Mkono wa kuume waBwana
umetenda mambo makuu!
16 Mkono wa kuume waBwana
umeinuliwa juu,
mkono wa kuume waBwana
umetenda mambo makuu!”
17 Sitakufa bali nitaishi,
nami nitatangaza yaleBwanaaliyoyatenda.
18 Bwanaameniadhibu vikali,
lakini hakuniacha nife.
19 Nifungulie malango ya haki,
nami nitaingia na kumshukuruBwana.
20 Hili ni lango laBwana
ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21 Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu,
umekuwa wakovu wangu.
22 Jiwe walilolikataa waashi,
limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 Bwanaametenda hili,
nalo ni la kushangaza machoni petu.
24 Hii ndiyo sikuBwanaaliyoifanya,
tushangilie na kufurahi ndani yake.
25 EeBwana, tuokoe,
EeBwana, utujalie mafanikio.
26 Heri yule ajaye kwa jina laBwana.
Kutoka katika nyumba yaBwanatunakubariki.
27 Bwanandiye Mungu,
naye ametuangazia nuru yake.
Mkiwa na matawi mkononi,
unganeni kwenye maandamano ya sikukuu
hadi kwenye pembe za madhabahu.
28 Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru,
wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29 MshukuruniBwanakwa kuwa ni mwema;
upendo wake wadumu milele.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/118-be933dac5034ae0b06fc0dc59d5bc913.mp3?version_id=1627—