Zaburi 126

Kurejeshwa Kutoka Utumwani

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Bwanaalipowarejeza mateka Sayuni,

tulikuwa kama watu walioota ndoto.

2 Vinywa vyetu vilijaa kicheko,

ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.

Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,

“Bwanaamewatendea mambo makuu.”

3 Bwanaametutendea mambo makuu,

nasi tumejaa furaha.

4 EeBwana, turejeshee watu wetu waliotekwa,

kama vijito katika Negebu.

5 Wapandao kwa machozi

watavuna kwa nyimbo za shangwe.

6 Yeye azichukuaye mbegu zake

kwenda kupanda,

huku akilia,

atarudi kwa nyimbo za shangwe,

akiwa ameyachukua

matita ya mavuno yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/126-911e1a86f635da446023b7d1d66d0b5f.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × one =