Bila Mungu, Kazi Ya Mwanadamu Haifai
(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Solomoni)
1 Bwanaasipoijenga nyumba,
wajengao hufanya kazi bure.
Bwanaasipoulinda mji,
walinzi wakesha bure.
2 Mnajisumbua bure kuamka mapema
na kuchelewa kulala,
mkitaabikia chakula:
kwa maana yeye huwapa usingizi
wapenzi wake.
3 Wana ni urithi utokao kwaBwana,
watoto ni zawadi kutoka kwake.
4 Kama mishale mikononi mwa shujaa
ndivyo walivyo wana
awazaao mtu katika ujana wake.
5 Heri mtu ambaye podo lake
limejazwa nao.
Hawataaibishwa wanaposhindana
na adui zao langoni.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/127-3d0950ea8f485d2b1b38b93607d112ef.mp3?version_id=1627—