Zaburi 130

Kuomba Msaada

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Kutoka katika vilindi ninakulilia, EeBwana,

2 EeBwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3 Kama wewe, EeBwana,

ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

EeBwana, ni nani

angeliweza kusimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 NamngojeaBwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6 Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7 Ee Israeli, mtumainiBwana,

maana kwaBwanakuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka katika dhambi zao zote.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/130-0fa0927afafceabcb36aa675010cc524.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

sixteen + 17 =