Wito Wa Kumsifu Mungu
(Wimbo Wa Kwenda Juu)
1 MsifuniBwana, ninyi nyote
watumishi waBwana,
ninyi mnaotumika usiku
ndani ya nyumba yaBwana.
2 Inueni mikono yenu katika mahali patakatifu
na mumsifuBwana.
3 NayeBwana, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/134-0ab0f077880d8b738f1866dcc6bb3977.mp3?version_id=1627—