Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

(Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

2 Uchukue ngao na kigao,

inuka unisaidie.

3 Inua mkuki wako na fumolako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Uiambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

4 Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu,

wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

5 Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika waBwanaakiwafukuza;

6 njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika waBwanaakiwafuatilia.

7 Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

8 maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

9 Ndipo nafsi yangu itashangilia katikaBwana

na kuufurahia wokovu wake.

10 Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, EeBwana?

Huwaokoa maskini kutokana na watu

walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana

na wanaowanyang’anya!”

11 Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza kwa mambo nisiyoyajua.

12 Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

13 Lakini walipokuwa wagonjwa,

nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

14 niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama vile ninayemwombolezea mama yangu.

15 Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

16 Kama watu wasiomcha Mungu wamedhihaki,

wamenisagia meno.

17 EeBwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

18 Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

19 Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

20 Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.

21 Hunifumbulia vinywa vyao wakisema,

“Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

22 EeBwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, EeBwana.

23 Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

24 Nihukumu kwa haki yako, EeBwanaMungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

25 Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

26 Wote wanaofurahia dhiki yangu

na waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

na wavikwe aibu na dharau.

27 Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

na wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote,

“Bwanaatukuzwe,

ambaye amefurahia

mafanikio ya mtumishi wake.”

28 Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/35-55cb7add9158b71d13574b9940749697.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

15 − 4 =