Mungu Yuko Pamoja Nasi
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora. Mtindo Wa Alamothi)
1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa
nayo milima ikiangukia moyoni wa bahari.
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka,
milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,
mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka,
Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka,
Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi,
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njoni mkaone kazi zaBwana
jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia,
anakata upinde na kuvunjavunja mkuki,
anateketeza ngao kwa moto.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu;
nitatukuzwa katikati ya mataifa,
nitatukuzwa katika dunia.”
11 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi;
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/46-2f02b0237beb5a914cb3b0cb7ee4c0f0.mp3?version_id=1627—