Zaburi 47

Mtawala Mwenye Enzi Yote

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora)

1 Pigeni makofi, enyi mataifa yote,

mpigieni Mungu kelele za shangwe!

2 Jinsi gani alivyo wa kutisha,BwanaAliye Juu Sana,

Mfalme mkuu juu ya dunia yote.

3 Ametiisha mataifa chini yetu

na mataifa chini ya miguu yetu.

4 Alituchagulia urithi wetu kwa ajili yetu

fahari ya Yakobo, aliyempenda.

5 Mungu amepaa katikati ya kelele za shangwe,

Bwanakatikati ya sauti za tarumbeta.

6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa,

mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.

7 Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote,

mwimbieni zaburi za sifa.

8 Mungu anatawala juu ya mataifa,

Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu.

9 Wakuu wa mataifa wanakusanyika kama watu wa Mungu wa Abrahamu,

kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu;

yeye ametukuka sana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/47-e21b9683f9512765cfa2895d3ed9ceab.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

8 + five =