Zaburi 52

Hukumu Ya Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Daudi Baada Ya Doegi, Mwedomu, Kumwendea Sauli Na Kumjulisha Kuwa Daudi Amekwenda Nyumbani Kwa Abimeleki)

1 Ewe jitu, mbona unajivunia ubaya?

Kwa nini unajivuna mchana kutwa,

wewe ambaye ni fedheha mbele za Mungu?

2 Ulimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi,

ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila.

3 Unapenda mabaya kuliko mema,

uongo kuliko kusema kweli.

4 Unapenda kila neno lenye kudhuru,

ewe ulimi wenye hila!

5 Hakika Mungu atakushusha chini

kwa maangamizi ya milele:

atakunyakua na kukuondoa kwa nguvu

kutoka katika hema yako,

atakung’oa kutoka nchi ya walio hai.

6 Wenye haki wataona na kuogopa,

watamcheka, wakisema,

7 “Huyu ni yule mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa ngome yake,

bali alitumainia wingi wa utajiri wake

na akawa hodari kwa kuwaangamiza wengine!”

Neema Ya Mungu

8 Lakini mimi ni kama mti wa mzeituni

unaostawi katika nyumba ya Mungu,

nautegemea upendo wa Mungu usiokoma

milele na milele.

9 Nitakusifu milele kwa yale uliyoyatenda,

nitatumaini jina lako, kwa kuwa jina lako ni jema.

Nitakusifu mbele ya watakatifu wako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/52-866b48522de5e9ba80791781fd94b645.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

sixteen − 8 =