Zaburi 54

Kuomba Ulinzi Wa Mungu Kutokana Na Adui

(Kwa Mwimbishaji Na Ala Za Nyuzi Za Uimbaji. Utenzi Wa Daudi Wakati Mtu Mmoja Wa Zifu Alipomwendea Sauli Na Kumjulisha Kuwa Daudi Amejificha Kwao)

1 Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,

unifanyie hukumu kwa uwezo wako.

2 Ee Mungu, sikia maombi yangu,

usikilize maneno ya kinywa changu.

3 Wageni wananishambulia,

watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,

watu wasiomjali Mungu.

4 Hakika Mungu ni msaada wangu,

Bwana ndiye anayenitegemeza.

5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,

kwa uaminifu wako uwaangamize.

6 Nitakutolea dhabihu za hiari;

EeBwana, nitalisifu jina lako

kwa kuwa ni vyema.

7 Kwa maana ameniokoa

kutoka katika shida zangu zote,

macho yangu yameona kwa furaha

ushindi dhidi ya adui zangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/54-d49c4c9ba5831ca660230c77e7a26ee4.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 + eighteen =