Zaburi 61

Kuomba Ulinzi

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Uimbaji. Zaburi Ya Daudi)

1 Ee Mungu, sikia kilio changu,

usikilize maombi yangu.

2 Kutoka miisho ya dunia ninakuita,

ninaita huku moyo wangu unadhoofika;

uniongoze kwenye mwamba

ule ulio juu kuliko mimi.

3 Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu,

ngome imara dhidi ya adui.

4 Natamani kukaa hemani mwako milele

na kupata kimbilio chini ya uvuli wa mbawa zako.

5 Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,

umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.

6 Mwongezee mfalme siku za maisha yake,

miaka yake kwa vizazi vingi.

7 Yeye na atawazwe kwenye kiti cha enzi

mbele za Mungu milele;

amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.

8 Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako

na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/61-3ac274c7c3493b29ad55324abf7cd5cb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 × 3 =