Zaburi 64

Kuomba Ulinzi Dhidi Ya Maadui

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Ee Mungu, unisikie, ninapoeleza lalamiko langu,

uyahifadhi maisha yangu kutokana

na vitisho vya adui.

2 Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu,

kutokana na zile kelele

za kundi la watenda mabaya.

3 Wanaonoa ndimi zao kama panga

na kuelekeza maneno yao

kama mishale ya kufisha.

4 Hutupa mishale kutoka kwenye mavizio

kwa mtu asiye na hatia,

humrushia ghafula bila woga.

5 Kila mmoja humtia moyo mwenzake

katika mipango mibaya;

huzungumza juu ya kuficha mitego yao,

nao husema, “Ni nani ataiona?”

6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,

“Tumebuni mpango mkamilifu!”

Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

7 Bali Mungu atawapiga wao kwa mshale,

nao utawapata ghafula na kuanguka.

8 Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao

na kuwaleta kwenye maangamizi;

wote wawaonao watatikisa vichwa vyao

kwa dharau.

9 Wanadamu wote wataogopa,

watatangaza kazi za Mungu

na kutafakari yale aliyoyatenda.

10 Wenye haki na wafurahi katikaBwana,

na wakimbilie kwake;

wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/64-0954e5e1243e91350d7b817e5d554bc1.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five × 4 =