Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu
(Kwa Mwimbishaji: Na Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi. Wimbo)
1 Mungu uturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wako,
2 ili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.
3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4 Mataifa yote na wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
6 Ndipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7 Mungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/67-2c582af6264c83c4cba031743f9b97c6.mp3?version_id=1627—