Zaburi 67

Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Na Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi. Wimbo)

1 Mungu uturehemu na kutubariki,

na kutuangazia nuru za uso wako,

2 ili njia zako zijulikane duniani,

wokovu wako katikati ya mataifa yote.

3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,

mataifa yote na wakusifu.

4 Mataifa yote na wafurahi na kuimba kwa shangwe,

kwa kuwa unatawala watu kwa haki

na kuongoza mataifa ya dunia.

5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,

mataifa yote na wakusifu.

6 Ndipo nchi itatoa mazao yake,

naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.

7 Mungu atatubariki

na miisho yote ya dunia itamcha yeye.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/67-2c582af6264c83c4cba031743f9b97c6.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five × four =