Zaburi 75

Mungu Ni Mwamuzi

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Uimbaji Za Nyuzi. Zaburi Ya Asafu. Wimbo)

1 Ee Mungu, tunakushukuru,

tunakushukuru wewe,

kwa kuwa jina lako li karibu;

watu husimulia matendo yako ya ajabu.

2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum;

ni mimi nihukumuye kwa haki.

3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka,

ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.

4 Kwa wale wenye majivuno ninasema,

‘Msijisifu tena’,

kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.

5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;

msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’ ”

6 Hakuna ye yote atokaye mashariki wala magharibi

au kutoka jangwani

awezaye kumkweza mwanadamu.

7 Bali Mungu ndiye ahukumuye:

Humshusha huyu na kumkweza mwingine.

8 Mkononi mwaBwanakuna kikombe

kilichojaa mvinyo unaotoka povu

uliochanganywa na vikolezo;

huumimina, nao waovu wote wa dunia

hunywa mpaka tone la mwisho.

9 Bali mimi, nitatangaza hili milele;

nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.

10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote,

bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/75-7aff16755558c333f90a5afc2d18b118.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

twelve + 17 =