Zaburi 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako

juu ya mbingu.

2 Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao

umeweka sifa,

kwa sababu ya watesi wako,

kuwanyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 Nikiziangalia mbingu zako,

kazi ya vidole vyako,

mwezi na nyota,

ulizoziratibisha,

4 mwanadamu ni kitu gani hata umkumbuke,

binadamu hata umwangalie?

5 Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu,

umemvika taji ya utukufu na heshima.

6 Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;

umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.

7 Kondoo, mbuzi na ng’ombe wote pia,

naam, na wanyama wa kondeni,

8 ndege wa angani na samaki wa baharini,

naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 EeBwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/8-9b9688e20a06c6dd7f5a4839406532c4.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

13 − one =