Zaburi 82

Maombi Kwa Ajili Ya Kutaka Haki

(Zaburi Ya Asafu)

1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,

anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:

2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki

na kuonyesha upendeleo kwa waovu?

3 Teteeni wanyonge na yatima,

tunzeni haki za maskini na walioonewa.

4 Mwokoeni mnyonge na mhitaji,

wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.

5 “Hawajui lo lote, hawaelewi lo lote.

Wanatembea gizani,

misingi yote ya dunia imetikisika.

6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;

ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’

7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;

mtaanguka kama mtawala mwingine ye yote.”

8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,

kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/82-60692687af86ed7e0cf29b48afb24c48.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

12 + 18 =