Zaburi 86

Kuomba Msaada

(Maombi Ya Daudi)

1 EeBwana, sikia na unijibu,

kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.

2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,

wewe ni Mungu wangu,

mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

3 EeBwana, nihurumie mimi,

kwa maana ninakuita mchana kutwa.

4 Mpe mtumishi wako furaha,

kwa kuwa kwako wewe, EeBwana,

ninainua nafsi yangu.

5 EeBwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,

umejaa upendo kwa wote wakuitao.

6 EeBwana, sikia maombi yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie.

7 Katika siku ya shida yangu nitakuita,

kwa maana wewe utanijibu.

8 EeBwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,

hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

9 EeBwana, mataifa yote uliyoyafanya

yatakuja na kuabudu mbele zako;

wataliletea utukufu jina lako.

10 Kwa maana wewe ni mkuu

na unafanya mambo ya ajabu;

wewe peke yako ndiwe Mungu.

11 EeBwana, nifundishe njia yako,

nami nitakwenda katika kweli yako;

nipe moyo usiositasita,

ili niweze kulicha jina lako.

12 EeBwana, wangu, nitakusifu kwa moyo wote;

nitaliadhimisha jina lako milele.

13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu;

# umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi.

14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia;

kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu:

watu wasiokuheshimu wewe.

15 Lakini wewe, EeBwana, ni Mungu wa huruma na neema,

si mwepesi wa hasira,

bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.

16 Nigeukie na unihurumie;

mpe mtumishi wako nguvu zako,

# mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.

17 Nipe ishara ya wema wako,

ili adui zangu waione nao waaibishwe,

kwa kuwa wewe, EeBwana,

umenisaidia na kunifariji.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/86-374bffae46feebf1d5ca5d4a064fa2db.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

five × 1 =