Zaburi 87

Sifa Za Yerusalemu

(Zaburi. Wimbo Wa Wana Wa Kora)

1 Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;

2 Bwanaanayapenda malango ya Sayuni

kuliko makao yote ya Yakobo.

3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako,

Ee mji wa Mungu:

4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabuna Babeli

miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:

# Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,

nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”

5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,

“Huyu na yule walizaliwa humo,

naye Aliye Juu Sana mwenyewe

atamwimarisha.”

6 Bwanaataandika katika orodha mataifa:

# “Huyu alizaliwa Sayuni.”

7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,

“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/87-b58571d086216174f2c1a99235746623.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

four × 4 =