Zaburi 96

Mungu Mfalme Mkuu

1 MwimbieniBwanawimbo mpya;

mwimbieniBwanadunia yote.

2 MwimbieniBwana, lisifuni jina lake;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu

miongoni mwa mataifa yote.

4 Kwa kuwaBwanani mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakiniBwanaaliziumba mbingu.

6 Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

7 MpeniBwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeniBwanautukufu na nguvu.

8 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;

leteni sadaka na mje katika nyua zake.

9 MwabuduniBwanakatika uzuri wa utakatifu wake;

dunia yote na itetemeke mbele zake.

10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwanaanatawala.”

Ulimwengu ameuweka imara

hauwezi kusogezwa,

atawahukumu mataifa kwa uadilifu.

11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

bahari na ivume,

na vyote vilivyomo ndani yake;

12 mashamba na yashangilie,

pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.

Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha,

13 vitaimba mbele zaBwana

kwa maana anakuja,

anakuja kuhukumu dunia.

Ataihukumu dunia kwa haki

na mataifa katika kweli yake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/96-a54c28136746e51ea86d1c4f8707af2d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

ten − 5 =