Zaburi 98

Mungu Mtawala Wa Dunia

1 MwimbieniBwanawimbo mpya,

kwa maana ametenda mambo ya ajabu;

kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu

umemfanyia wokovu.

2 Bwanaameufanya wokovu wake ujulikane

na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.

3 Ameukumbuka upendo wake

na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli;

miisho yote ya dunia imeuona

wokovu wa Mungu wetu.

4 Mpigieni kelele za shangwe, dunia yote,

ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;

5 mwimbieniBwanakwa kinubi,

kwa kinubi na sauti za kuimba,

6 kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu

za pembe za kondoo dume:

shangilieni kwa furaha mbele zaBwana,

aliye Mfalme.

7 Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake,

dunia na wote wakaao ndani yake.

8 Mito na ipige makofi,

milima na iimbe pamoja kwa furaha,

9 vyote na viimbe mbele zaBwana,

kwa maana yuaja kuhukumu dunia.

Atahukumu dunia kwa haki

na mataifa kwa haki.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/98-7163a39f7828c4519ba46a2a4ee3a38a.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

7 + fourteen =