Ayubu 40

1 Bwanaakamwambia Ayubu: 2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.” 3 Ndipo Ayubu akamjibuBwana: 4 “Mimi sistahili kabisa, ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu. 5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.” 6 NdipoBwanaakasema na Ayubu kutoka katika upepo […]

Ayubu 41

1 “Je, waweza kumvua Lewiathanikwa ndoano ya samaki au kufunga ulimi wake kwa kamba? 2 Waweza kupitisha kamba puani mwake au kutoboa taya lake kwa kulabu? 3 Je, ataendelea kukuomba umhurumie? Atasema nawe maneno ya upole? 4 Je, atafanya agano nawe ili umtwae awe mtumishi wako maisha yake yote? 5 Je, utamfuga na kumfanya rafiki […]

Ayubu 42

Ayubu Anamjibu Bwana 1 Ndipo Ayubu akamjibuBwana: 2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika. 3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua. 4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa […]

Esta 1

Malkia Vashti Aondolewa 1 Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahusuero ambaye alitawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi mpaka Kushi. 2 Wakati huo Mfalme Ahusuero alipotawala katika kiti chake cha enzi kilikuwa katika ngome ya mji wa Shushani, 3 Katika mwaka wa tatu wa kutawala kwake, alifanya […]

Esta 2

Esta Afanywa Malkia 1 Baadaye, wakati hasira ya Mfalme Ahusuero ilipokuwa imetulia, alimkumbuka Vashti na kile alichokuwa amekifanya na alilokuwa ameamuru juu yake. 2 Kisha watumishi waliomhudumia mfalme walipendekeza, “Na ufanyike utafiti kwa ajili ya wanawali mabikira wazuri wa sura kwa ajili ya mfalme. 3 Mfalme na ateue maafisa katika kila jimbo la himaya yake […]

Esta 3

Hila Ya Hamani Kuwaangamiza Wayahudi 1 Baada ya matukio haya, Mfalme Ahusuero alimheshimu Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, akampandisha na kumpa kiti chake cha heshima cha juu sana kuliko wakuu wengine wote. 2 Maafisa wote wa kifalme waliokaa langoni mwa mfalme walipiga magoti na kumpa Hamani heshima, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru hili kuhusu Hamani. […]

Esta 4

Mordekai Amshawishi Esta Kusaidia 1 Wakati Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu. 2 Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna ye yote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia. 3 Katika kila jimbo ambapo […]

Esta 5

Ombi La Esta Kwa Mfalme 1 Siku ya tatu Esta alivaa mavazi yake ya kimalkia, naye akasimama katika ua wa ndani wa jumba la mfalme, mbele ya ukumbi wa mfalme. Naye mfalme alikuwa akiketi katika kiti chake cha kifalme katika ukumbi, akielekea langoni. 2 Alipomwona Malkia Esta amesimama uani alipendezwa naye, akamnyoshea fimbo ya utawala […]

Esta 6

Mordekai Anapewa Heshima 1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe. 2 Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumwua Mfalme Ahusuero. 3 Mfalme akauliza, “Je, ni […]

Esta 7

Hamani Aangikwa 1 Basi mfalme na Hamani wakaenda kula chakula pamoja na Malkia Esta, 2 walipokuwa wakinywa mvinyo katika siku ya pili, mfalme akauliza tena, “Malkia Esta, ni nini haja yako? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.” 3 Kisha Malkia Esta akajibu, “Kama nimepata kibali kwako, Ee mfalme, tena kama inapendeza […]