Zaburi 129

Maombi Dhidi Ya Adui Wa Israeli

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2 wamenionea mno tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3 Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4 LakiniBwanani mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5 Wale wote waichukiao Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6 Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8 Wale wapitao karibu na wasiseme,

“Baraka yaBwanaiwe juu yako;

tunakubariki katika jina laBwana.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/129-9ffa949f38b7f78e6764c6dbb56706d0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

three × one =