Maombi Dhidi Ya Adui Wa Israeli
(Wimbo Wa Kwenda Juu)
1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4 LakiniBwanani mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.
5 Wale wote waichukiao Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Wawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka yaBwanaiwe juu yako;
tunakubariki katika jina laBwana.”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/129-9ffa949f38b7f78e6764c6dbb56706d0.mp3?version_id=1627—