Zaburi 128

Thawabu Ya Kumtii Bwana

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Heri ni wale wote wamchaoBwana,

waendao katika njia zake.

2 Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

katika nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchayeBwana.

5 Bwanana akubariki kutoka Sayuni

siku zote za maisha yako,

na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6 nawe ujaliwe kuishi

uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/128-42322bf991cd46273a32779b87cfd157.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

12 + one =