Zaburi 127

Bila Mungu, Kazi Ya Mwanadamu Haifai

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Solomoni)

1 Bwanaasipoijenga nyumba,

wajengao hufanya kazi bure.

Bwanaasipoulinda mji,

walinzi wakesha bure.

2 Mnajisumbua bure kuamka mapema

na kuchelewa kulala,

mkitaabikia chakula:

kwa maana yeye huwapa usingizi

wapenzi wake.

3 Wana ni urithi utokao kwaBwana,

watoto ni zawadi kutoka kwake.

4 Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana

awazaao mtu katika ujana wake.

5 Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/127-3d0950ea8f485d2b1b38b93607d112ef.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 × 3 =