Zaburi 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Wale wamtumainioBwanani kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika wadumu milele.

2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyoBwanaanavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili kwamba wenye haki wasije

wakatumia mikono yao

kutenda ubaya.

4 EeBwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwanaatawafukuza

pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/125-370cee1374973ac54166d030d902839e.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two × five =