Zaburi 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 KamaBwanaasingalikuwa upande wetu;

Israeli na aseme sasa:

2 kamaBwanaasingalikuwa upande wetu,

wakati watu walipotushambulia,

3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,

wangalitumeza tungali hai,

4 Mafuriko yangalitugharikisha,

maji mengi yangalitufunika,

5 maji yaendayo kasi

yangalituchukua.

6 Bwanaasifiwe,

yeye ambaye hakuruhusu

turaruliwe kwa meno yao.

7 Tumeponyoka kama ndege

kutoka katika mtego wa mwindaji;

mtego umevunjika,

nasi tukaokoka.

8 Msaada wetu ni katika jina laBwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/124-9ccb6bbd9ae29a84ffb8315500236917.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × 3 =