Zaburi 123

Kuomba Rehema

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe ambaye

kiti cha enzi kiko mbinguni.

2 Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mtumishi wa kike

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyoBwanaMungu wetu,

mpaka atakapotuhurumia.

3 Uturehemu, EeBwana, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4 Tumevumilia dhihaka nyingi

kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi

kutoka kwa wenye majivuno.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/123-731c2710bf4366fcd14b363a09c0ebe6.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

6 + 16 =