Kuomba Rehema
(Wimbo Wa Kwenda Juu)
1 Ninayainua macho yangu kwako,
kwako wewe ambaye
kiti cha enzi kiko mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumwa
yatazamavyo mkono wa bwana wao,
kama vile macho ya mtumishi wa kike
yatazamavyo mkono wa bibi yake,
ndivyo macho yetu yamtazamavyoBwanaMungu wetu,
mpaka atakapotuhurumia.
3 Uturehemu, EeBwana, uturehemu,
kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
4 Tumevumilia dhihaka nyingi
kutoka kwa wenye kiburi,
dharau nyingi
kutoka kwa wenye majivuno.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/123-731c2710bf4366fcd14b363a09c0ebe6.mp3?version_id=1627—