Zaburi 122

Sifa Kwa Yerusalemu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,

“Twende katika nyumba yaBwana.”

2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama

malangoni mwako.

3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji

ambao umeshikamanishwa pamoja.

4 Huko ndiko makabila hukwea,

makabila yaBwana,

kulisifu jina laBwanakulingana na maagizo

waliopewa Israeli.

5 Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa,

viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.

6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:

“Wote wakupendao na wawe salama.

7 Amani na iwepo ndani ya kuta zako

na usalama ndani ya ngome zako.”

8 Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki,

nitasema, “Amani iwe ndani yako.”

9 Kwa ajili ya nyumba yaBwanaMungu wetu,

nitatafuta mafanikio yako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/122-e9675173996f9bd2375b6b4776caf398.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × two =