Zaburi 121

Bwana Mlinzi Wetu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Nayainua macho yangu nitazame vilima,

msaada wangu utatoka wapi?

2 Msaada wangu hutoka kwaBwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

3 Hatauacha mguu wako uteleze,

yeye akulindaye hatasinzia,

4 hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

5 Bwanaanakulinda,

Bwanani uvuli wako mkono wako wa kuume,

6 jua halitakudhuru mchana,

wala mwezi wakati wa usiku.

7 Bwanaatakukinga na madhara yote,

atayalinda maisha yako,

8 Bwanaatakulinda unapoingia na unapotoka,

tangu sasa na hata milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/121-8f6089c6e8e51612f7206e5112f479e0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

thirteen + thirteen =