Bwana Mlinzi Wetu
(Wimbo Wa Kwenda Juu)
1 Nayainua macho yangu nitazame vilima,
msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu hutoka kwaBwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
3 Hatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,
4 hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.
5 Bwanaanakulinda,
Bwanani uvuli wako mkono wako wa kuume,
6 jua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.
7 Bwanaatakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,
8 Bwanaatakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/121-8f6089c6e8e51612f7206e5112f479e0.mp3?version_id=1627—