Zaburi 120

Kuomba Msaada

(Wimbo Wa Kwenda Juu)

1 Katika dhiki yangu namwitaBwana,

naye hunijibu.

2 EeBwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo

na ndimi za udanganyifu.

3 Atakufanyia nini,

au akufanyie nini zaidi,

Ewe ulimi mdanganyifu?

4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,

kwa makaa yanayowaka

ya mti wa mretemu.

5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,

kwamba naishi katikati

ya hema za Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno

miongoni mwa wale

wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani;

lakini ninaposema,

wao wanataka vita.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/120-df46a67e829af36a3dad513361f137eb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

3 × two =