Zaburi 114

Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri

1 Wakati Israeli walipotoka Misri,

nyumba ya Yakobo

kutoka kwa watu wa lugha ngeni,

2 Yuda akawa makao matakatifu ya Mungu,

Israeli akawa milki yake.

3 Bahari ilitazama ikakimbia,

Yordani ulirudi nyuma,

4 milima ilirukaruka kama kondoo waume,

vilima kama wana-kondoo.

5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,

Ee Yordani, nawe ukarudi nyuma,

6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo waume,

enyi vilima, kama wana-kondoo?

7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,

mbele za Mungu wa Yakobo,

8 yeye aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,

mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/114-a52b5ed5bf63e707f5cbb4eefbbfdc14.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × 3 =