Bwana Na Mfalme Wake Mteule
(Zaburi Ya Daudi)
1 Bwanaamwambia Bwana wangu:
“Keti mkono wangu wa kuume,
mpaka nitakapowafanya adui zako
kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
2 Bwanaataeneza fimbo yako ya utawala
yenye nguvu kutoka Sayuni;
utatawala katikati ya adui zako.
3 Askari wako watajitolea kwa moyo
katika siku yako ya vita.
Ukiwa umevikwa fahari takatifu,
kutoka kwenye tumbo la mapambazuko
# utapokea umande wa ujana wako.
4 Bwanaameapa,
naye hatabadilisha mawazo yake:
“Wewe ni kuhani milele,
kwa mfano wa Melkizedeki.”
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume,
atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
6 Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga
na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
7 Atakunywa maji katika kijito kando ya njia,
kwa hiyo atainua kichwa chake juu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/110-8f324b599490c012590b4eb9baf7390b.mp3?version_id=1627—