Zaburi 102

Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu

(Maombi Ya Mtu Aliyechoka, Anayeteseka, Anayemimina Malalamiko Kwa

Bwana

)

1 EeBwana, usikie maombi yangu,

kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.

2 Usinifiche uso wako

ninapokuwa katika shida.

Unitegee sikio lako,

ninapoita, unijibu kwa upesi.

3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,

mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.

4 Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,

ninasahau kula chakula changu.

5 Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,

nimebakia ngozi na mifupa.

6 Nimekuwa kama bundi wa jangwani,

kama bundi kwenye magofu.

7 Nilalapo sipati usingizi,

nimekuwa kama ndege mpweke

kwenye paa la nyumba.

8 Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,

wale wanaonizunguka

hutumia jina langu kama laana.

9 Ninakula majivu kama chakula changu

na nimechanganya kinywaji changu na machozi

10 kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,

kwa maana umeniinua na kunitupa kando.

11 Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,

ninanyauka kama jani.

12 Lakini wewe, EeBwana,

umeketi katika kiti chako cha enzi milele,

sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.

13 Utainuka na kuihurumia Sayuni,

kwa maana ni wakati

wa kumwonyesha wema;

wakati uliokubalika umewadia.

14 Kwa maana mawe yake ni ya thamani

kwa watumishi wako,

vumbi lake lenyewe hulionea huruma.

15 Mataifa wataogopa jina laBwana,

wafalme wote wa dunia

watauheshimu utukufu wako.

16 Kwa maanaBwanaataijenga tena Sayuni

na kutokea katika utukufu wake.

17 Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,

wala hatadharau hoja yao.

18 Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,

ili taifa litakaloumbwa baadaye

waweze kumsifuBwana:

19 “Bwanaalitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,

kutoka mbinguni alitazama dunia,

20 kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa

na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”

21 Kwa hiyo jina laBwanalatangazwa huko Sayuni

na sifa zake katika Yerusalemu,

22 wakati mataifa na falme zitakapokusanyika

kumwabuduBwana.

23 Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,

akafupisha siku zangu.

24 Ndipo niliposema:

“Ee Mungu wangu,

usinichukue katikati ya siku zangu;

miaka yako inaendelea vizazi vyote.

25 Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,

na mbingu ni kazi ya mikono yako.

26 Hivi vitatoweka, lakini wewe utadumu,

vyote vitachakaa kama vazi.

Utavibadilisha kama nguo

navyo vitaondoshwa.

27 Lakini wewe, U yeye yule,

nayo miaka yako haikomi kamwe.

28 Watoto wa watumishi wako

wataishi mbele zako;

wazao wao wataimarishwa

mbele zako.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/102-dc2ab09e05dc7cba3ad9c246c7c4d214.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fourteen − eight =