Zaburi 99

Mungu Mfalme Mkuu

1 Bwanaanatawala,

mataifa na yatetemeke;

anaketi kwenye kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

2 Bwanani mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

4 Mfalme mwenye nguvu hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

5 MtukuzeniBwanaMungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita naye aliwajibu.

7 Alizungumza nao kutoka katika nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

8 EeBwana, wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9 MtukuzeniBwanaMungu wetu

na mwabudu kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maanaBwanaMungu wetu ni mtakatifu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/99-11d9d4ae955a940aed5492da831339ad.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eighteen + 16 =