Sifa Za Yerusalemu
(Zaburi. Wimbo Wa Wana Wa Kora)
1 Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 Bwanaanayapenda malango ya Sayuni
kuliko makao yote ya Yakobo.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako,
Ee mji wa Mungu:
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabuna Babeli
miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:
# Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,
nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,
“Huyu na yule walizaliwa humo,
naye Aliye Juu Sana mwenyewe
atamwimarisha.”
6 Bwanaataandika katika orodha mataifa:
# “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,
“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/87-b58571d086216174f2c1a99235746623.mp3?version_id=1627—