Zaburi 84

Kuionea Shauku Nyumba Ya Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Wana Wa Kora)

1 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

makao yako yapendeza kama nini!

2 Nafsi yangu inatamani sana,

naam, hata kuona shauku,

kwa ajili ya nyua zaBwana;

moyo wangu na mwili wangu

vinamlilia Mungu Aliye Hai.

3 Hata shomoro amejipatia makao,

mbayuwayu amejipatia kiota

mahali awezapo kuweka makinda yake:

mahali karibu na madhabahu yako,

EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

Mfalme wangu na Mungu wangu.

4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,

wanaokusifu wewe daima.

5 Heri ni wale ambao nguvu zao ziko kwako,

na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

6 Wanapopita katika Bonde la Baka,

hulifanya mahali pa chemchemi,

# pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.

7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu,

hadi kila mmoja afikapo

mbele za Mungu huko Sayuni.

8 EeBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote,

sikia maombi yangu;

nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.

9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu,

mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.

10 Siku moja katika nyua zako ni bora

kuliko siku elfu mahali pengine;

afadhali ningekuwa bawabu

katika nyumba ya Mungu wangu

kuliko kukaa katika mahema ya waovu.

11 Kwa kuwaBwanani jua na ngao,

Bwanahutoa wema na heshima;

hakuna kitu chema anachowanyima

wale ambao hawana hatia.

12 EeBwanaMwenye Nguvu Zote,

heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/84-de9fa6d217312710ae91c4f248286a9d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × three =