Zaburi 70

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Maombolezo)

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa,

EeBwana, njoo hima unisaidie.

2 Waaibike na kufedheheshwa

wale wanaotafuta uhai wangu;

wale wanaotamani kuangamizwa kwangu

warudishwe nyuma kwa aibu.

3 Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4 Lakini wote wakutafutao

na washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako daima na waseme,

“Mungu na atukuzwe!”

5 Hata sasa mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

EeBwana, usikawie.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/70-098f2b592afdfeb0c290fdafa03c8c88.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

18 − 16 =