Zaburi 53

Uovu Wa Wanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Utenzi Wa Daudi)

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 Mungu huwachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wo wote wanaomtafuta Mungu.

3 Kila mmoja amegeukia mbali,

wameharibika wote pamoja,

hakuna hata mmoja atendaye mema,

naam! Hata mmoja.

4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza,

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

na ambao hawamwiti Mungu?

5 Hapo watatetemeka kwa hofu kuu,

ambapo hakuna cha kutetemesha.

Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;

umewaaibisha, kwa sababu Mungu amewadharau.

6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni!

Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/53-b53885ea57ed4462561650e8e252af99.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two × three =