Zaburi 46

Mungu Yuko Pamoja Nasi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Wana Wa Kora. Mtindo Wa Alamothi)

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,

msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa

nayo milima ikiangukia moyoni wa bahari.

3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka,

milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.

4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,

mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.

5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka,

Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka,

Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.

7 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8 Njoni mkaone kazi zaBwana

jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia,

anakata upinde na kuvunjavunja mkuki,

anateketeza ngao kwa moto.

10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu;

nitatukuzwa katikati ya mataifa,

nitatukuzwa katika dunia.”

11 BwanaMwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi;

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/46-2f02b0237beb5a914cb3b0cb7ee4c0f0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

four × two =