Zaburi 34

Sifa Na Wema Wa Mungu

(Zaburi Ya Daudi, Alipojifanya Mwendawazimu Mbele Ya Abimeleki, Ambaye Alimfukuza, Naye Akaondoka)

1 NitamtukuzaBwananyakati zote,

sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.

2 Nafsi yangu itajisifu katikaBwana

walioonewa wasikie na wafurahi.

3 MtukuzeniBwanapamoja nami,

naam, na tulitukuze jina lake pamoja.

4 NilimtafutaBwananaye akanijibu,

akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

5 Wale wamtazamao hutiwa nuru,

nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

6 Maskini huyu alimwitaBwanaakamsikia,

akamwokoa katika taabu zake zote.

7 Malaika waBwanahufanya kituo

akiwazunguka wale wamchao,

naye huwaokoa.

8 Onjeni mwone kwambaBwanani mwema,

heri mtu yule anayemkimbilia.

9 McheniBwanaenyi watakatifu wake,

kwa maana wale wamchao

hawapungukiwi na kitu cho chote.

10 Wana simba wenye nguvu

hutindikiwa na kuona njaa,

bali wale wamtafutaoBwana

hawatakosa kitu cho chote kilicho chema.

11 Njoni, watoto wangu, mnisikilize,

nitawafundisha kumchaBwana.

12 Ye yote kati yenu anayependa maisha

na kutamani kuziona siku nyingi njema,

13 auzuie ulimi wake na mabaya

na midomo yake kutokana

na kusema uongo.

14 Aache uovu na atende mema,

aitafute amani na kuifuatia.

15 Macho yaBwanayako kwa wenye haki

na masikio yake yako makini

kusikia kilio chao;

16 uso waBwanauko kinyume na watenda mabaya,

kufuta kumbukumbu lao duniani.

17 Wenye haki hulia, nayeBwanahuwasikia,

huwaokoa katika taabu zao zote.

18 Bwanayu karibu nao waliovunjika moyo

na huwaokoa waliopondeka roho.

19 Mwenye haki ana mateso mengi,

lakiniBwanahumwokoa nayo yote,

20 huhifadhi mifupa yake yote,

hata mmoja hautavunjika.

21 Ubaya utamwua mtu mwovu,

adui za mwenye haki watahukumiwa.

22 Bwanahuwakomboa watumishi wake,

wale wanaomkimbilia yeye

hawatahukumiwa hata mmoja wao.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/34-ccb420443dc43577cc3db3894086b01d.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nineteen − 9 =