Isaya 57

Ibada Ya Sanamu Ya Israeli Iliyo Batili

1 Mwenye haki hupotea,

wala hakuna hata mmoja

awazaye hilo moyoni mwake;

watu wanaomcha Mungu huondolewa,

wala hakuna hata mmoja anayeelewa

kuwa wenye haki wameondolewa

wasipatikane na maovu.

2 Wale waendao kwa unyofu

huwa na amani;

hupata pumziko walalapo mautini.

3 “Lakini ninyi, njoni hapa, ninyi wana wa wachawi,

ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!

4 Mnamdhihaki nani?

Ni nani mnayemcheka kwa dharau

na kumtolea ndimi zenu?

Je, ninyi si watoto wa waasi,

Uzao wa waongo?

5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni

na chini ya kila mti uliotanda matawi;

mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde

na chini ya majabali yenye mianya.

6 “Sanamu zilizoko katikati ya mawe laini ya mabondeni

ndiyo fungu lenu;

hizo ndizo sehemu yenu.

Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji,

na kutoa sadaka za nafaka.

Kwa ajili ya haya yote,

niendelee kuona huruma?

7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka,

huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.

8 Nyuma ya milango yako na miimo yako

umeweka alama zako za kipagani.

Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako,

umepanda juu yake

na kukipanua sana;

ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao,

nawe uliangalia uchi wao.

9 Ulikwenda kwa Molekiukiwa na mafuta ya zeituni

na ukaongeza manukato yako.

Ukawatuma wajumbe wako mbali sana,

# ukashuka kwenye kaburilenyewe!

10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote,

lakini usingeliweza kusema,

‘Hakuna tumaini.’

Ulipata uhuisho wa nguvu zako,

kwa sababu hiyo hukuzimia.

11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa

hata ukaniambia uongo,

wala hukunikumbuka

au kutafakari hili moyoni mwako?

Si kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu

kwamba huniogopi?

12 Nitaifunua haki yako na matendo yako,

nayo hayatakufaidia.

13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada,

sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe!

Upepo utazipeperusha zote,

pumzi peke yake itazipeperusha,

Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake,

atairithi nchi

na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”

Faraja Kwa Wenye Majuto

14 Tena itasemwa:

“Jengeni, jengeni, itengenezeni njia!

Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”

15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu,

yeye aliyeinuliwa sana,

yeye aishiye milele,

ambaye jina lake ni Mtakatifu:

“Ninaishi mimi mahali palipoinuka

tena palipo patakatifu,

tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu

na mwenye roho ya unyenyekevu,

ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu

na kuihuisha mioyo yao waliotubu.

16 Sitaendelea kulaumu milele,

wala sitakasirika siku zote,

kwa kuwa roho ya mwanadamu

ingezimia mbele zangu:

yaani pumzi ya mwanadamu niliyemwumba.

17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi;

nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira,

yeye bado aliendelea katika njia zake za tamaa.

18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya,

nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,

19 nikiumba sifa katika midomo ya waombolezaji

katika Israeli.

Amani, amani, kwa wale walio mbali

na kwa wale walio karibu,”

asemaBwana. “Nami nitawaponya.”

20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo,

ambayo haiwezi kutulia,

mawimbi yake hutupa takataka na matope.

21 Mungu wangu asema,

“Hakuna amani kwa waovu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/57-5d612401288fe3f4bde3fa1583fde07c.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

sixteen − fourteen =